Wajina huyo ndio mwanamke yule penny dumu gani hata changamoto hana,wema ni mzuri,mvumilivu,anjua kuhandle,miss independent,anakupenda,mta futaji,mpenda maendeleo,japo mliachana ww ndio uliongea mbovu but xio yy cheki ulimletea dharau pale Mlimani city,pia ktk cm lkn hakujali anaongea wazi anakupenda Naseeb,take care boy she loves you very much,mtafute mtoto na huyo mrembo hakuna mwanamke anayekuweza zaid ya huyo......
Reply · 16 · Like · Follow Post · 9 hours ago
Tuma neno PERUZI kwenda 15368 kupata habari za bongo Movies sasa. Wateja wa Vodacom Pekee
“Umemwona Wema, kwa sasa ana ngozi nzuri yenye afya na iliyo na mng’aro kama alivyokuwa awali,ni nzuri sana yani, ameacha kabisa kutumia dawa za kung’arisha ngozi hilo ndilo lililonivutia zaidi kwani alisikiliza ushauri niliompa kabla.”
Hiyo ni kauli ya staa aliyetikisa mwaka 2013 bwana Diamond Platnumz aliyoitoa hivi karibuni alipokuwa akizungumza na gazeti maarufu la michezo nchini hivi karibuni.
Diamond amesema Wema ndiye mwanamke anayetamani kuwa naye katika maisha yake, hivyo kauli yake aliyoitoa mwanzo kuhusu kuzaa na Wema ipo mbioni kutimia.
“Miezi kadhaa nyuma niliongea kuhusu nia yangu ya kuzaa na Wema, wakati huo nilikuwa bado na Penny, siwezi kukimbia kivuli changu kwani ukweli unabaki palepale nampenda yule binti, japokuwa wapo wanaosema kwamba sijatulia au natafuta ‘kiki’ kupitia warembo hawa, si kweli, Wema nilikuwa naye kabla ya Penny na vigezo vyangu ni mchumba anayejali kazi yangu na kujua kwamba mimi ni staa nahitajika sehemu yoyote, muda wowote, Wema ni mwelewa.” Alisisitiza Diamond