Jay Z ameripotiwa kumwambia rafiki yake wa karibu kuwa yeye na mkewe Beyonce Knowles na mtoto wao hawatahudhuria katika ndoa ya swahiba wake Kanye West itakayofanyika mwezi ujao jijini Paris Ufaransa.

Sababu za kutohudhuria ndoa hiyo zimeelezwa kuwa ni kutokana na tukio hilo kupangwa kuoneshwa kwenye reality show ya Keeping Up with the Kardashians.

Hata hivyo, chanzo kimeliambia gazeti la The Sun kuwa Jay Z amepanga kuwafanyia party kubwa baada ya tukio hilo itakayofanyika New York kwenye club yake ‘Club 40/40’ na kwamba amepanga kutumia kiasi cha  £100,000 katika honeymoon yao kama zawadi yake.

“Instead he's making it up to his mate by throwing him the most extravagant bachelor party known to man. It will cost a small fortune - and to top it all off, he's chucked a £100 000 yacht rental in there as a wedding gift as well.” Kimeeleza chanzo hicho katika maelezo yake.
 
Top