Fanya kuangalia picha za utengenezaji wa video ya wimbo wa Chege na Temba "Wauwe" ambayo imeshutiwa ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere 
Katika video hiyo, Chege na Temba wamewapa shavu Jokate Mwegelo na aliekuwa mshiriki wa BBA Julio ambao wametokea kama marubani wa ndege, huku picha zingine zikiwaonyesha Chege na Temba wakiwa katika ndege hiyo.

Ukiangalia picha hizo utagundua kuwa mtengenezaji wa video hiyo ni Adam Juma, ambae alishawahi kutangaza kuachana na kazi ya utengenezaji wa video za muziki.










 
Top