FKB_0843

Miss Tanzania Photogenic 2014, Evelyn Baasa.
FKB_3067
 Warembo waliofanikiwa kuingia hatua ya tano bora ya
Redd’s Miss Tanzania Photogenic 2014, wakiwa katika picha ya pamoja na mshindi   wa taji hilo, Evelyn Baasa (katiakti) jana. Wengine kutoka kushoto ni Nicole  Sarakikya, Lilian Kamazima, Lilian Timothy na Dorice Mollel.

FKB_3031
 Warembo wakilisakata rumba kabla ya kuatangzwa kwa matokeo hayo.
 Baadhi ya warembo wakipiga picha ya pamoja na mshindi huyo wa Taji la Miss Tanzania Photogenic 2014
FKB_3078
MlimbwendeEvelyn Baasa (19) jana aliibuka kidedea kati ya walimbwende wenzake 30 na  kutwaa taji la Redds Miss Photogenic 2014.
Kwa kushinda taji hilo Baasa ambaye alinzania mbio za taji la Miss Tanzania katika Kitongoji cha Karatu naabadae kuingia Miss Arusha na Kanda ya Kaskazini amekuwa   mrembo wa kwanza kuingia Nusu Fainali ya mashindano Miss Tanzania 2014. 
Shindano hilo ni moja kati ya mataji matano ambayo yanashindaniwa na warembo hao ambapo  washindi wake wanapata tiketi ya kuingia Nusu Fainali ya shindano hilo litakalo  fanyika mapema mwezi ujao. 
 
Miongoni mwa mataji hayo ni Miss Tanzania Photogenic, Miss Tanzania Top Model, Miss   Tanzania Personality, Miss Tanzania Sports Lady na Miss Tanzania Talent.Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Lino International Agency, waandaaji wa Shindano la Miss   Tanzania, Hashim Lundenga ‘Uncle’ amesema jopo la majaji watatu ambao ni wapiga  picha na wadau wa masuala ya urembo  wa masuala ya urembo Tanzania walikaa na kumchagua mshindi huyo kupitia picha mbalimbali za warembo hao.
Majaji  waliowezesha kupatikana kwa mshindi huyo ni Mpigapicha mkongwe wa masuala ya urembo nchini Mroki Mroki ambaye anafanyakazi na Magazeti ya Serikali ya Daily News na Habarileo, Mtayarishaji wa vipindi Elliud Pemba wa True Vision na Afisa Itifaki Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha, Mukhsin Kassim.
Taji la Redd’s Miss Tanzania Photogenic lilikuwa linashikiliwa na Redd’s Miss Tanzania  2013 Happyness Watimanywa.Warembo wengine waliofanikiwa kuingia hatua ya tano bora ya Miss Photogenic ni Dorice Mollel, Nicole Sarakikya, Lilian Timothy na Lilian Kamazima.
Kesho warembo hao watachuana tena kuwania taji la Miss Top Model katika shindano litakalofanyika Triple A jijini Arusha
 
Top